Sunday, October 14, 2012

WANANCHI WA MLILIA MAGUFULI



Na Magreth Chaba
Karagwe.
Baadhi ya wakazi wa wilaya ya Karagwe wamemuomba waziri wa ujenzi Daktari John Magufuli kumulika zoezi la ulipaji fidia kupisha ujenzi wa barabara ya Kyaka – Bugene yenye urefu wa Km. 69.1 kwa madai kuwa uthamini wa mali ulifanyika kwa upendeleo.
Wananchi wa vijiji vya Kihanga na Kishao walitoa malalamiko hayo baada ya kubainika kwenye orodha ya watakaolipwa fidia zao nyumba zilizojengwa miaka ya karibuni na nyumba zilizojengwa  zaidi ya miaka 100 zikiondolewa katika orodha ya kufidiwa.
Mmoja wa wakazi wa kijiji cha Kishao Clement Nsherenguzi (76) alisema kuwa baadhi ya majirani walio na ardhi bila mazao katika eneo la mita 22.5 wamepewa fidia, na watu waliojenga hivi karibuni miaka michache wamepewa ambapo aliongeza kuwa zoezi la tathimini na utoaji wa fidia limeghubikwa na ahrufu ya huongo na rushwa.
“Sijui wanatumia vigezo na sheria gani katika kutoa fidia wazazi wangu wameishi hapa tangu mwaka 1880 na baadhi ya mibuni ilipandwa. Mwaka 1920, mimi mwenyewe nimezaliwa mwaka 1935 sasa naitwa mvamizi wa barabara mimi na barabara nani mvamizi? Alisema Nsherenguzi.
Alisema kwamba, migomba yake 300 mibuni 50 vyenye thamani ya shilingi 15,960,000/= viko kwenye orodha ya kufyekwa bila fidia ni pamoja na kiwanja ploti EE. 35 alichogawiwa na Halmashauri ya wilaya ambacho kinampa kodi kila mwaka katika eneo la Kayanga.
Naye mkazi wa kijiji hicho Magreth Peter (70) ambaye ni mama mjane alisema ameelezwa na Tanroads mkoa wa kagera kuwa nyumba yake itabomolewa bila fidia wakati huo jirani zake ambao wako ndani ya mita 22.5 kama yeye wakiwa wameanza kulipwa.
Mwananchi mwingine wa kijiji hicho Adventina Furuka (69) ambaye pia ni mjane alishangazwa na baadhi ya nyumba za kifahari zilizojengwa miaka ya karibuni katika kijiji hicho kuonekana katika orodha ya watakaolipwa huku wao majina yao yakikosekana.
“ Kwa mtindo huu rushwa  katika nchi hii itatumaliza kama waziri mwenye dhamana kama hataingilia haraka uthaminishaji uliofanyika katika barabara ya Kyaka – Bugene inayojengwa kwa kipande cha lami Alisema furuka.
Pia waliowatuhumu walioendesha zoezi la utathimini baada ya kudaiwa kuwataka  wamiliki wa nyumba za zamani kupeleka uthibitisho wa stakabadhi za kununua mabati ya kuezekea ili waingizwe kwenye orodha ya watakaofidiwa.
Kwa upande wake mzee Joseph Lwiza alidai zoezi la uthamini lilijaa mazingira yenye utata kwani baadhi ya wananchi waliitwa kwa ajili ya majadiliano na walioendesha zoezi hilo.
Aidha alisema majirani zake walioko, kwenye mita zile wameanza kupokea malipo huku yeye akijulishwa kuwa hatalipwa.

No comments:

Post a Comment