Monday, October 1, 2012

WAGONJWA WATAABIKA,DUKALA DAWA LAFUGWA



      Na  Magreth Chaba.
MAMLAKA ya dawa na chakula Tanzania [TFDA]imefunga duka la madawa katika hospitali teule ya wilaya ya Biharamulo mkoani Kagera baada ya duka hilo kuendeshwa bila ya kuwa na mfamasia wa kulihudumia.
Duka hilo limefungwa tangu Agosti mwaka huu na kusababisha usumbufu mkubwa kwa wagonjwa wanaofika hospitalini hapo ambao kutokana na hali hiyo wamekuwa wakilazimika kwenda kununua dawa kwenye maduka ya watu binafsi.
Kwa mujibui wa mganga mkuu wa hospitali hiyo Dk.Grasimus Sebuyoya,alisema duka hilo limejengwa kwa thamani ya zaidi ya sh.12 milion na kwamba  limefungwa likiwa na dawa yenye thamani ya sh.30 millon.
Alisema kuwa uongozi wa hospitali hiyo ulifikia uamuzi wa kuanzisha duka hilo kutokana na bohari ya dawa nchini[msd] kushindwa kupeleka dawa kwa ajili ya kuwahudumia wagonjwa ambao wamekuwa wakisumbuka kwenda kununua dawa hizo nje ya hospitali hiyo.
Pia,Dk.Sebuyoya alisema lengo la kuanzisha duka hilo ilikuwa kusaidia wagonjwa waliojiunga katika mifuko ya bima ya afya CHF na NHIF kwa lengo la kuwaondolea usumbufu wa kutafuta dawa Kutokana na uhaba wa dawa kutoka Msd unaoikabili hospitali hiyo.
Alisema mamlaka ya dawa na chakula[TFDA]ilifunga duka hilo kutokana na kukosa mfamasia wa kulisimamia.
‘’Tulipolianzisha tulitegemea mfamasia wa halmashauri atakuwa msimamizi wa hilo duka lakini imekuwa tofauti,tulivyokuwa tumetarajia na sisi hapa hatuna mfamisia wa kulisimamia duka hilo,mpango uliopo tunatafuta mfamisia Atakayekithi kiwango ili alisimamie,tuendeleze huu mradi wetu’’alisema Dk.Sebuyoya.
Aidha Dk.Sebuyoya aliongeza kuwa kutokana na changamoto hiyo makundi maalumu hususa ni akina mama wajawazito,watoto chini ya umri wa miaka 5,wazee na watu wenye magonjwa sugu wamekuwa wakilazimika kununua dawa kwenye maduka ya watu binafsi kinyume na tamko serikali la kutoa kuhuduma bure kwao.
‘’Serikali inasema tutoe huduma kwa makundi hayo bure,lakini inashindikana,maana bohari wana muda mrefu hawaleti dawa kwa maana hiyo tuna tatizo kubwa sana la ukosefu wa madawa na sisi tuliamua kuanzisha duka hili ili tuwasaidie wagonjwa wawe wanapata dawa karibu’’
Alisema hosiptali hiyo haijapokea dawa kutoka bohari ya Taifa tangu mwezi wa tatu mwaka huu na kwamba hali hiyo imekuwa ikiwalazimu wagongwa wanaofika katika hospitali hiyo wakiwemo watoto chini ya miaka mitano,wajawazito,na wazee kwenda kununua dawa hizo mitaani.
                                                                      MWISHO.                                                                   

No comments:

Post a Comment