Tuesday, October 23, 2012



WAKRISTO GEITA WACHARUKA WADAI HAWAKO TAYARI KUCHOMEWA MAKANISA
Na
MAGRETH CHABA
UMOJA wa makanisa ya kikristo ya Katoro wilayani Geita na Buseresere wilayani Chato,mkoani Geita umecharuka na kulaani kitendo cha hivi karibuni kilichofanywa na baadhi ya waumini wa dini ya kiislamu cha kuchoma moto makanisa na kuharibu mali za wakiristo.

Kitendo hicho kilisababisha vurugu kubwa zilizotokea  oktoba 12 mwaka huu Mbagala Kizuiani jijini Dar es Salaam ambapo makanisa saba yalichomwa moto kutokana na kitendo kinachodaiwa na mtoto mwenye umri wa miaka 14 kukojolea Quran.

Umoja huo umetoa tamko kuhusiana na kitendo hicho katika mkutano wa uliofanyika juzi mjini Katoro na kuwakutanisha waumini wa madhehebu mbalimbali ya kikristo pamoja na viongozi wao.

Akitoa tamko hilo mwenyekiti wa umoja huo,Mchungaji Joseph Mwanzalima Hewa,alisema serikali ikishindwa kudhibiti matukio ya vurugu za waislamu kujichukulia sheria mkononi kutokana na udini taifa halitakuwa na amani.

Alisema kuna hatari ya taifa,linaweza kuingia katika umwagaji wa damu kwani kitendo hicho hakivumiliki kwa wakristo kuzidi kupumbazika kwa kuharibiwa mali zao.

Hewa alisema zaidi ya biblia 50 ziliwahi kuchomwa moto lakini wakristo hawakuchukua hatua zozote dhidi ya wahusika wala hakuna msikiti uliochomwa moto na kwamba hakuna vurugu zilizotokea na hivyo kuhoji uhalali wa waislamu kuiweka nchi kwenye rehani ya vita ya kidini.

Alisema serikali inapaswa kuingilia kati kukomesha matukio hayo yanayofanywa na baadhi ya makundi ya waumini wa dini ya kiislamu ili nchi iendelee kuwa kisiwa cha amani.

Aidha alisema kama serikali itashindwa kudhibiti matukio hayo,hawatavumilia kuendelea kuharibiwa makanisa yao na kudai kuwa wako tayari kufa wakitetea haki zao.

Kiongozi huyo aliongeza kuwa waliohusika katika matukio hayo wanapaswa kuchukulia hatua kali za kisheria akiwemo kinara wa kikundi cha Uamsho kisiwani Zanzibar Sheikh Farid Hadi Ahmed.

''Serikali imekuwa ikiwakumbatia waislamu sasa tunasema yatosha,hatuwezi kuona mali zetu zinaharibiwa,kama itakuwa kimiya katika hili nchi itaingia katika vurugu kubwa na vita kutokana na udini ulioanza kujipenyeza''alisema Hewa.

Naye aliyewahi kuwa mwenyekiti wa umoja huo Isaya Ikili alisema anasikitishwa na watendaji wa kata pamoja na viongozi wa serikali kushindwa kuhudhuria katika mkutano huo licha kupewa mwaliko ili kujua matamko yao.

Alisema wako tayari kupambana na maadui wao wanaoharibu makanisa yao na kwamba polisi wasiingilie vurugu hizo kama serikali itashindwa kuyadhibiti.
                                                                            MWISHO.

MW/KITI CCM GEITA APIGWA STOP MGODINI AKIENDA KUZINDUA KAMPENI
Na                           
Magreth chaba

VIGOGO wa chama cha mapinduzi(ccm)mkoani Geita waliochaguliwa hivi karibuni ,akiwemo mwenyekiti wa mkoani ,Joseph Msukuma wameonja machungu ya mgodi wa dhahabu wa Geita (GGM)baada ya msafara wao kuzuiliwa kwa muda wakati wakielekea kwenye uzinduzi wa kampeni za uchaguzi mdogo.

Tukio la kuzuiliwa kwa viongozi hao lilitokea jana mchana saa 7:03 kutokana na kile kilichodaiwa na walinzi wa mgodi huo kampuni ya G4S waliokuwa wamefura hawakuwa na taarifa za viongozi hao kupita mgodini hapo kitendo kilichosababisha majibizano makali ya maneno kati ya walinzi hao na vigogo hao.

Mwenyekiti huyo alikumbwa na kizazaa hicho akiwa na katibu wa itikadi na uenezi mkoa Said Kalidushi na katibu wa uchumi na fedha mkoa Malugu Mwendesha walipokuwa wakielekea katika kuzindua  kampeni za uchaguzi mdogo wa kata ya Lwezera tarafa ya Bugando.

Baada ya kuzuiliwa Msukuma alijitambulisha kwa walinzi kuwa ni mwenyekiti wa ccm mkoa huku akiwaonyesha bendera ya chama iliyokuwa ikipepea kwenye gari lake lenye namba za usajili T 164 AFQ aina ya Toyota V-8 lakini walinzi walisema wao wanafuata sheria za uongozi wa mgodi huo na kwamba hawakuwa tayari kuruhu kupita kwa kuwa hawakupewa na taarifa.

Msukuma alisikika akiwakaripia maneno walinzi hao’’serikali Unayoitaka wewe ni ipi,tueleweshe ama unataka ya chama gani huoni hata bendera,kila siku napita hapa huwa hamnioni na hili gari ’’

Naye mlinzi mmoja alisikika akisema’’sisi tunafuata taratibu zilizopo,kwani mnaelekea wapi?,sisi hata kama ni kiongozi wa serikali anapofika hapa huwa tunataarifiwa lakini sasa hatuJajulishwa’’

Kufuatia maneno hayo ya mwenyekiti,mlinzi mmoja alijitokeza na kulazimika kupiga simu mgodini kuuliza kuhusu kumruhusu kupita ambapo wakati akifanya mawasiliano hayo mlinzi huyo alisikika akizitaya namba za gari hilo.

Mlinzi huyo baada ya kuwasiliana na uongozi wa mgodi huo na kuruhusiwa viongozi hao kupita saa 7:25,mmoja wao alisema’’tunaomba samahani kama tumewachelewesha sisi tunafuata taratibu za uongozi wa mgodi’’.

Aidha akiwa katika uzinduzi wa kampeni hizo mwenyekiti wa aliwataka wananchi wa kata hiyo kumchagua mgombea wa ccm Misango Jeremiah ili kuwaletea maendeleo katika kata hiyo ikiwemo huduma ya afya barabara na ofisi ya kata hiyo.

Kampeni za uchaguzi huo unaotarajia kufanyika oktoba 28 mwaka huu unakuja kufuatia kifo cha aliyekuwa diwani wa kata hiyo Anatori Mkufu aliyefariki februari 23,mwaka huu kwa ajali ya gari akiwa jijini Mwanza.
                                                                    MWISHO.

WAKRISTO GEITA WACHARUKA WADAI HAWAKO TAYARI KUCHOMEWA MAKANISA



WAKRISTO GEITA WACHARUKA WADAI HAWAKO TAYARI KUCHOMEWA MAKANISA
Na
MAGRETH CHABA
UMOJA wa makanisa ya kikristo ya Katoro wilayani Geita na Buseresere wilayani Chato,mkoani Geita umecharuka na kulaani kitendo cha hivi karibuni kilichofanywa na baadhi ya waumini wa dini ya kiislamu cha kuchoma moto makanisa na kuharibu mali za wakiristo.

Kitendo hicho kilisababisha vurugu kubwa zilizotokea  oktoba 12 mwaka huu Mbagala Kizuiani jijini Dar es Salaam ambapo makanisa saba yalichomwa moto kutokana na kitendo kinachodaiwa na mtoto mwenye umri wa miaka 14 kukojolea Quran.

Umoja huo umetoa tamko kuhusiana na kitendo hicho katika mkutano wa uliofanyika juzi mjini Katoro na kuwakutanisha waumini wa madhehebu mbalimbali ya kikristo pamoja na viongozi wao.

Akitoa tamko hilo mwenyekiti wa umoja huo,Mchungaji Joseph Mwanzalima Hewa,alisema serikali ikishindwa kudhibiti matukio ya vurugu za waislamu kujichukulia sheria mkononi kutokana na udini taifa halitakuwa na amani.

Alisema kuna hatari ya taifa,linaweza kuingia katika umwagaji wa damu kwani kitendo hicho hakivumiliki kwa wakristo kuzidi kupumbazika kwa kuharibiwa mali zao.

Hewa alisema zaidi ya biblia 50 ziliwahi kuchomwa moto lakini wakristo hawakuchukua hatua zozote dhidi ya wahusika wala hakuna msikiti uliochomwa moto na kwamba hakuna vurugu zilizotokea na hivyo kuhoji uhalali wa waislamu kuiweka nchi kwenye rehani ya vita ya kidini.

Alisema serikali inapaswa kuingilia kati kukomesha matukio hayo yanayofanywa na baadhi ya makundi ya waumini wa dini ya kiislamu ili nchi iendelee kuwa kisiwa cha amani.

Aidha alisema kama serikali itashindwa kudhibiti matukio hayo,hawatavumilia kuendelea kuharibiwa makanisa yao na kudai kuwa wako tayari kufa wakitetea haki zao.

Kiongozi huyo aliongeza kuwa waliohusika katika matukio hayo wanapaswa kuchukulia hatua kali za kisheria akiwemo kinara wa kikundi cha Uamsho kisiwani Zanzibar Sheikh Farid Hadi Ahmed.

''Serikali imekuwa ikiwakumbatia waislamu sasa tunasema yatosha,hatuwezi kuona mali zetu zinaharibiwa,kama itakuwa kimiya katika hili nchi itaingia katika vurugu kubwa na vita kutokana na udini ulioanza kujipenyeza''alisema Hewa.

Naye aliyewahi kuwa mwenyekiti wa umoja huo Isaya Ikili alisema anasikitishwa na watendaji wa kata pamoja na viongozi wa serikali kushindwa kuhudhuria katika mkutano huo licha kupewa mwaliko ili kujua matamko yao.

Alisema wako tayari kupambana na maadui wao wanaoharibu makanisa yao na kwamba polisi wasiingilie vurugu hizo kama serikali itashindwa kuyadhibiti.
                                                                            MWISHO.

MW/KITI CCM GEITA APIGWA STOP MGODINI AKIENDA KUZINDUA KAMPENI
Na                           
Magreth chaba

VIGOGO wa chama cha mapinduzi(ccm)mkoani Geita waliochaguliwa hivi karibuni ,akiwemo mwenyekiti wa mkoani ,Joseph Msukuma wameonja machungu ya mgodi wa dhahabu wa Geita (GGM)baada ya msafara wao kuzuiliwa kwa muda wakati wakielekea kwenye uzinduzi wa kampeni za uchaguzi mdogo.

Tukio la kuzuiliwa kwa viongozi hao lilitokea jana mchana saa 7:03 kutokana na kile kilichodaiwa na walinzi wa mgodi huo kampuni ya G4S waliokuwa wamefura hawakuwa na taarifa za viongozi hao kupita mgodini hapo kitendo kilichosababisha majibizano makali ya maneno kati ya walinzi hao na vigogo hao.

Mwenyekiti huyo alikumbwa na kizazaa hicho akiwa na katibu wa itikadi na uenezi mkoa Said Kalidushi na katibu wa uchumi na fedha mkoa Malugu Mwendesha walipokuwa wakielekea katika kuzindua  kampeni za uchaguzi mdogo wa kata ya Lwezera tarafa ya Bugando.

Baada ya kuzuiliwa Msukuma alijitambulisha kwa walinzi kuwa ni mwenyekiti wa ccm mkoa huku akiwaonyesha bendera ya chama iliyokuwa ikipepea kwenye gari lake lenye namba za usajili T 164 AFQ aina ya Toyota V-8 lakini walinzi walisema wao wanafuata sheria za uongozi wa mgodi huo na kwamba hawakuwa tayari kuruhu kupita kwa kuwa hawakupewa na taarifa.

Msukuma alisikika akiwakaripia maneno walinzi hao’’serikali Unayoitaka wewe ni ipi,tueleweshe ama unataka ya chama gani huoni hata bendera,kila siku napita hapa huwa hamnioni na hili gari ’’

Naye mlinzi mmoja alisikika akisema’’sisi tunafuata taratibu zilizopo,kwani mnaelekea wapi?,sisi hata kama ni kiongozi wa serikali anapofika hapa huwa tunataarifiwa lakini sasa hatuJajulishwa’’

Kufuatia maneno hayo ya mwenyekiti,mlinzi mmoja alijitokeza na kulazimika kupiga simu mgodini kuuliza kuhusu kumruhusu kupita ambapo wakati akifanya mawasiliano hayo mlinzi huyo alisikika akizitaya namba za gari hilo.

Mlinzi huyo baada ya kuwasiliana na uongozi wa mgodi huo na kuruhusiwa viongozi hao kupita saa 7:25,mmoja wao alisema’’tunaomba samahani kama tumewachelewesha sisi tunafuata taratibu za uongozi wa mgodi’’.

Aidha akiwa katika uzinduzi wa kampeni hizo mwenyekiti wa aliwataka wananchi wa kata hiyo kumchagua mgombea wa ccm Misango Jeremiah ili kuwaletea maendeleo katika kata hiyo ikiwemo huduma ya afya barabara na ofisi ya kata hiyo.

Kampeni za uchaguzi huo unaotarajia kufanyika oktoba 28 mwaka huu unakuja kufuatia kifo cha aliyekuwa diwani wa kata hiyo Anatori Mkufu aliyefariki februari 23,mwaka huu kwa ajali ya gari akiwa jijini Mwanza.
                                                                    MWISHO.

Monday, October 22, 2012

RAS GEITA:KISUKARI KINAHARIBU BAJETI YA SERIKALI.



RAS GEITA:KISUKARI KINAHARIBU BAJETI YA SERIKALI.

NA
Magreth Chaba

KATIBU tawala wa mkoa wa Geita,Severine Kahitwa amesema magonjwa ya kisukari,presha na ukimwi ni magonjwa ambayo yamekuwa yakiharibu mpango wa bajeti ya serikali kwa sababu magonjwa hayo hutibiwa kwa muda mrefu.

Alisema hali hiyo inatokana na kuongezeka kwa magonjwa yasiyo ambukiza hapa nchini na kuwa tishio katika maisha ya binadamu kwa kupunguza muda wa kuishi na ubora wa maisha pamoja na kuathiri maendeleo ya Taifa.

Rai hiyo ilitolewa leo(jana) kwenye uzinduzi wa mradi wa afya ya jamii kwa wakazi wa mji wa Geita unaotekelezwa na shirika la Amref kwa ushirikiano na kampuni ya Mgodi wa Geita GGM na Halmashauri ya wilaya ya Geita.

Katibu tawala alisema magonjwa hayo yamekuwa tishio kubwa hapa nchini na kwamba serikali imekuwa ikitumia fedha nyingi kuhudumia wagonjwa wanakumbwa na magonjwa hao na hivyo jamii kuitaka kuwa na tabia ya kijitokeza kupima afya kila wakati.

Akisoma hotuba yake alisema magonjwa hayo yamekuwa yakienea kwa kasi kutokana na mfumo wa maisha ambayo mtu huamua kuishi na hasa kuhusu vyakula anavyotumia,mazoezi ya mwili na kujijengea tabia zisizoaa kiafya.

Kufuatia hali hiyo,Kahitwa amewataka wananchi kuachana na vyakula vya kisasa vyenye mafuta mengi na badala yake kutumia vyakula vya asili ili kuondokana na hatari ya kukumbwa na magonjwa hayo ambayo yamekuwa yakitibiwa kwa gharama kubwa na kwa muda mrefu.

Shirika la Amref kwa kushirikiana na kampuni ya mgodi wa Geita GGM na halmashauri ya wilaya ya Geita unatekeleza mradi huo unalenga kupima magonjwa mbalimbali yakiwemo yasiyo ya kuambukiza,kama kisukari,presha,ugonjwa wa kinywa na meno pamoja na magonjwa ya zinaa na ukimwi.

Kaimu ofisa mradi huo Potence Mhaya,akielezea mradi huo alisema katika hatua ya uzinduzi mradi huo utatekelezwa katika kata ya Kalangalala na Mtakuja kwenye kijiji cha Nyakabare na kwamba huduma hiyo itaendelea kutolewa kwenye kila kituo cha afya.

Hata hivyo baadhi ya watu waliojitokeza jana kwenye siku ya uzinduzi wameomba serikali kuboresha huduma ya afya na kuondoa tatizo la uhaba wa dawa ambalo licha ya wao kujitokeza kupima na kugudulika kuwa magonjwa dawa za matibabu changamoto kwao.
                                           MWISHO
                                                  

Sunday, October 21, 2012

FISI WAZIDI KULETA MADHARA KWA BINADAMU GEITA

FISI wamezidi kuleta madhara kwa binadamu katika mkoa wa Geita,kufuatia wanawake wawili wakazi wa Kitongoji cha Ndati kijiji cha Shabaka wilaya ya Nyang'hwale kunusurika kuuawa baada ya kushambuliwa na wananyama hao waliovamia makazi yao usiku wa manane kisha kuwajeruhi vibaya,mwanamke mmoja akiachwa bila kiganja cha mkono.

Matukio hayo yametokea siku chache baada ya mtoto Hawa Baltazari(5)kukamatwa na kuliwa na fisi katika kijiji jirani cha Nyakato kata ya Nyanguku wilayani Geita saa moja usiku wa kuamkia septemba 21 mwaka huu.

Mtoto huyo alinyakuliwa na fisi akiwa anatoka kujisaidia umbali wa mita 50 kutoka nyumba ya bibi yake aitwaye Mariamu Bwegera(65) ambaye alikuwa akiishi na mtoto huyo enzi za uhai wake.

Wanawake hao ambao mmoja amelazwa katika hospitali ya wilaya ya Geita wametambulika kwa majina ya Janeti Lukas(21)ambaye alijeruhiwa vibaya usoni,kichwani,Tumboni na kukatwa kiganja cha mkono wa kushoto na Laurencia Lubatula(38)amejeruhiwa mkono wa kushoto kwa kukwaruzwa na kucha za wanayama hao.

Matukio ya kushambuliwa wanawake hao yametokea saa 8:30 usiku wa kuamkia octoba 16 mwaqka huu baada ya fisi hao kugonga milango kwa nguvu kisha kuingia ndani ya nyumba za  familia mbili tofauti kisha kuwashambulia wakati wanawake hao wakijihami kunusuru watoto wao wachanga wasiliwe na wanyama hao.

Akizungumza  Mwenyekiti wa kitongoji cha Ndati  Kamuli Mashauri alisema kabla ya kutokea kwa matukio hayo makundi ya fisi yamekuwa yakionekana mara kwa mara katika kijiji hicho wakitafuta chakula hasa nyakati za jioni
Naye majeruhi wa tukio hilo Janet Lukas aliye lazwa   wodi namba nane ya majeruhi   amesema kabla ya kushambuliwa,fisi huyo alimjeruhi mume wake mguuni na baada ya kukimbia kwenda kuomba msaada kwa majirani fisi huyo aliiingia ndani na kuanza kumshambulia huku akiwa amemkumbatia mtoto wake Pendo Ayubu mwenye umri wa miezi tisa ili asiliwe na fisi.

Fisi huyo aliuawa na babu yake na Janeti aliyefika kutoa msaada baada ya kumpiga kwa shoka kichwani.

kwa upande wake Mganga wa zamu katika hospitali ya wilaya Geita aliye zungumza na mwandishi wa habari hizi Dk.Adam Sijaona alisema wanawake walipokelewa wakiwa katika hali mbaya kutokana na majeraha ya kucha za wanyama hao lakini baada ya kupatiwa matibabu wanaendelea vizuri na kwamba mmoja wao ameruhisiwa kwenda nyumbani baada ya kupatiwa matibabu.

Aidha mwanamke Raulencia Lubatula alijeruhiwa wakati akinusuru mifugo wake wasishambuliwa ambapo fisi huyo alikuwa ameuwa mbuzi wawili na kondoo mmoja.

Akithibisha kutokea kwa matukio hayo ofisa wanayama pori wa wilaya ya Geita na Nyang'hwale Samweli Mwita alisema kuzagaa kwa fisi hao kunatokana na uharibifu wa mazingira katika hifadhi ya mistu baada ya watu kujihusisha na uchomaji wa mikaa,kupasua mbao kilimo na kukata magogo.

Amesema wanayama hao wanapokosa sehemu ya kujihifadhi hulazimika kuzagaa kwenye makazi ya watu wakitafuta chakula na maji na hivyo wanapokuwa katika hatua hiyo ndipo wamekuwa wakisababisha madhara hao.

Aidha amesema jumla ya watoto sita wenye umri wa kati ya miaka mitano na sita wamekufa baada ya kuuawa na fisi kwenye kata za Nyanguku,Busolwa,Kakora,Nayarugusu,Lwezera na Nyijundu katika kipindi cha kuanzia april hadi oktoba mwaka huu,huku fisi 20 wanaodaiwa kuhusika katika matukio hayo wameuawa na askari wa kuzuia ujangiri.

Top of Form
Bottom of Form