Tuesday, October 2, 2012

AFYA ZA MAJERUHI WA BASI LILO TEKETEA KWA MOTO ZAENDELEA VIZURI



Na

Magreth chaba


BIHARAMULO

HALI za majeruhi waliolazwa katika Hospitali teule ya wilaya ya Biharamulo kutokana na ajali ya basi lilliloteketea kwa moto katika kijiji cha Nyantakala wilayani Biharamulo mkoani Kagera zimeelezwa kuendelea vizuri huku mmoja kati yao akiwa ameruhusiwa.
Mganga mkuu wa hospitali hiyo Grasimus Sebuyoya amesema hali zao zinaendelea vizuri ikilinganishwa na hali zao walipokuwa wanapokelewa katika hospitali hiyo.
Majeruhi aliyeruhusiwa ametambulika kwa jina la Msigwa Isaya[22]mkazi wa Katoro mkoani Geita ambaye ni mwanafunzi wa shule ya sekondari Kigoma.
 Majeruhi wanaoendelea kupata matiobabu katika hospitali hiyo ni Phinihas Elias[37]mwalimu wa shule ya sekondari Shamaliwa Igoma jijini Mwanza,Pius John[21]askari wa JWT kikosi cha 24 kj Kigoma,Johary Chapa[23]Mkazi wa Kwimba mkoani Mwanza,Josephina Ngereza[46]Kasulu ,Rashidi Mahonda[48]Kasulu  na Elies Ngereza[60]kazi wa kasulu wote wakiwa wameungua moto sehemu mbalimbali za miili yao.
Majeruhi wengine ni  Dotto Tryphone[30]mkazi wa Nyakanazi na Zainabu Issa(23)Mkazizi wa kigoma  ambao wote wamevunjika miguu ya kushoto.
Ajali hiyo ilitokea jana saa 4:30 asubuhi na kulihusisha basi la kampuni ya Adventure lenye namba T 293 BDP Aina ya Nissani Diseal ambalo lilikuwa likitokea mkoani Mwanza kwenda mkoani Kigoma.
Aidha Kamanda wa polisi mkoa wa Kagera,Philip Kalangi alisema chanzo cha ajali hiyo ni kutokana na hitilafu kwenye mfumo wa umeme na kuongeza kuwa uchunguzi wa ajali hiyo unaendelea.
Hata hivyo kauli hiyo ya kamanda imetofautia na baadhi ya abiria wa basi hilo na mashuhuda wa ajali ambao walisema huenda baadhi yao waliungulia ndani ya basi hilo hasa watoto na wazee ambao walishindwa kujinusuru kutoka ndani ya basi hilo.
Kalangi alikanusha madai ya kutokea Vifo katika ajali hiyo isipokuwa mali zilizokuwemo ziliteketea kwa moto na kwamba abiria walionusurika katika ajali hiyo walisafirishwa na basi jingine.
                                             MWISHO.

No comments:

Post a Comment