Friday, March 2, 2012

TUTUNZE MAZINGIRA

                                                                                                    


Baadhi ya wananchi wakifanya  usafi katika mazingira ya makazi yao kutokana na utupaji wa taka ovyo unao changia uharibifu wa mazingira na kuharibu uoto wa asili





Mazingira ni vitu vyote vilivyopo katika uoto wa asili ikiwa ni pamoja na wanyama ,mimea, maji wadudu na udongo, kuwa vitu hivi vyote vina sitahili kuhifadhiwa ili kutunza mazingira.

Hifadhi ya mazingira katika maisha ya binadamu ni jambo la msingi  viumbe hai wanategeneza maisha yake kutokana na ubora wa uhifadhi wa mazingira, rangi ya umbijani katika mazingira huvutia na kuongeza ubora wa hewa safi kwa viumbe hai.

Jamii nyingi hapa nchini wameshindwa kuhifadhi mazingira kutokana na  kuwepo kwa nishati duni kwani wananchi hukata miti ovyo uchomaji wa mistu na hali hiyo imesababisha uharibifu wa mazingira kwani asilimia 80 wanaishi vijijini ambako hakuna nishati mbadala.

Uharibifu wa mazingira umechangia kuporomoka kwa uchumi kutokana na sehemu kubwa ya nchi kuwa jangwa jambo ambalo huchangia uzalishaji kuwa duni .

Aidha vitu vingine vinavyo changia uharibifu wa mazingira ni viwanda vingi kujengwa katikati ya makazi ya watu na kuchangia kuwepo kwa hali ya ukaa na kuathiri hali ya hewa na Afya za binadamu,ni pamoja na baadhi ya jamii za kitanzania kufuga mifugo wengi ambao nao pia huchangia uharibifu wa mazingira kwa kusababisha mmomonyoko wa udongo.




No comments:

Post a Comment