Thursday, March 1, 2012

TUDUMISHE MILA ZETU TUACHANE NA MILA ZA KIGENI

Katika kudumisha mila na tamaduni zetu hizi ni baadhi ya ngoma za jadi  zilizotumika na zinaendelea kutumika  katika utamaduni mwa mwafrika katika kudumisha mila na desturi hutumika wakati wa sherehe, matukio ya hatari na katika mikutano na awali zititumika kuwa burudisha machifu .

Ngoma hizo hupatikana katika miji ya watu binafsi ,ofisi za vijiji na katika majumba ya makumbusho mbalimbali yaliyopo hapa nchini kama vile BUDAP iliyopo eneo la Nyamkazi  Bukoba Mjini,Bwera nyange Wilayani Karagwe ,Kiyanja, Kiziba, Kyamtwara Bujora Mwanza na sehemu nyinginezo hapa nchini  zilizo kuwa ni Makao Makuu ya Machifu.

Tamaduni hizi zinapaswa kuendelezwa kwani jamii nyingi zimeanza kudharau tamaduni na kushabikia tamaduni za kigeni, kwani ngoma hizi zilihamasisha mila na desturi katika jamii

Aidha ngoma hizi hutengenezwa kwa kutumia Ngozi za wanyama wanaofugwa katika jamii zetu na wakati mwingine huiingizia jamii kipatp kutoka na mauzo ya ngozi na ngoma zinazo tengenezwa.



 

No comments:

Post a Comment