Saturday, December 15, 2012
KITUO CHA POLISI MUGOMA NGARA CHATEKEKETEA,NA WATU WATATU WADAIWA KUPOTEZA MAISHA
Kituo cha police Mugoma wilayani ngara mkoani kagera kikiwa kimechomwa moto na wananchi,baada ya asikari police kumuua mkazi mmoja kwa risasi na hivyo kusababisha vurugu zilizopelekea asikari wawili Cpl Paschal & Pc Alex.
Mungu azipumzishe kwa amani roho zao marehemu waliotokana na tukio hili
Monday, November 26, 2012
JWTZ LA TOA UFAFANUZI MLIPUKO NGARA
JWTZ LATOA UFAFANUZI MLIPUKO NGARA.
Na
Magreth chaba ,Ngara
JESHI la wananchi wa Tanzania JWTZ kikosi cha Faru makao makuu ya Tabora limetoa ufafanuzi juu ya msihndo mkubwa uliojitokeza wilayani ngara mkoani kagera na kusababisha baadhi ya wananchi kuyakimbia kwa muda makazi yao kwa kuhofia maisha kutokana na kile walichodai bomu lilidondoka kwenye kijiji cha Ruganzo wilayani humo.
Katika tukio hilo ambalo lilitokea usiku wa Novemba 22 majira ya saa nane lilisababisha baadhi ya wakazi wa wilaya ya ngara kuishi kwa hofu kubwa kutokana kitu kisichofahamika kudondoka toka angani na kusababisha mshindo mkubwa mithili ya tetemeko la ardhi hali iliyopelekea baadhi ya nyumba kupata nyufa.
Kufuatia hali hiyo kiongozi wa kikosi cha JWTZ Mnadhimu mkuu wa mafunzo na utendaji wa kivita Brigedia ya Faru Kanali Simon Lali Hongoa amelazimika kutoa ufafanuzi wa kitu hicho baada ya wataalamu wa mabomu kufika kijiji cha Ruganzo kata ya Kibimba wilayani Ngara na kufanya uchunguzi wa kina baada ya kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya hiyo kushindwa kubaini ni kitu gani pamoja na madhara yake.
JESHI la wananchi wa Tanzania JWTZ kikosi cha Faru makao makuu ya Tabora limetoa ufafanuzi juu ya msihndo mkubwa uliojitokeza wilayani ngara mkoani kagera na kusababisha baadhi ya wananchi kuyakimbia kwa muda makazi yao kwa kuhofia maisha kutokana na kile walichodai bomu lilidondoka kwenye kijiji cha Ruganzo wilayani humo.
Katika tukio hilo ambalo lilitokea usiku wa Novemba 22 majira ya saa nane lilisababisha baadhi ya wakazi wa wilaya ya ngara kuishi kwa hofu kubwa kutokana kitu kisichofahamika kudondoka toka angani na kusababisha mshindo mkubwa mithili ya tetemeko la ardhi hali iliyopelekea baadhi ya nyumba kupata nyufa.
Kufuatia hali hiyo kiongozi wa kikosi cha JWTZ Mnadhimu mkuu wa mafunzo na utendaji wa kivita Brigedia ya Faru Kanali Simon Lali Hongoa amelazimika kutoa ufafanuzi wa kitu hicho baada ya wataalamu wa mabomu kufika kijiji cha Ruganzo kata ya Kibimba wilayani Ngara na kufanya uchunguzi wa kina baada ya kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya hiyo kushindwa kubaini ni kitu gani pamoja na madhara yake.
Kanali
Hongoa alikanusha vikali madai ya wananchi wa ngara kuwa kitu kilichodondoka
wilayani humo kilikuwa ni bomu la kivita na kudai kuwa maneno hayo hayakuwa na
ukweli wowote kwa kuwa kilichodondoka kilikuwa ni kipande cha setelaiti
iliyokuwa ikisafiri angani na inahofiwa kiliishiwa nguvu na kudodoka
katika eneo hilo.
Aidha alidai kuwa uchunguzi wa kitaalamu umebainisha kuwa setelaiti hiyo haina madhara yoyote na wala haikutoka uelekeo wa nchi jirani zinazoendelea na migogoro ya kivita kama baadhi ya maelezo ya wananchi wa wilaya hiyo walivyodai.
Aidha alidai kuwa uchunguzi wa kitaalamu umebainisha kuwa setelaiti hiyo haina madhara yoyote na wala haikutoka uelekeo wa nchi jirani zinazoendelea na migogoro ya kivita kama baadhi ya maelezo ya wananchi wa wilaya hiyo walivyodai.
Hangoa
alisema pamoja na kutokuwepo madhara kila mwananchi anatakiwa kuchukua tahadhari
ya kubeba vitu wasivyokuwa na uhakika navyo wakilenga kutaka kupata utajiri wa
haraka ambao unaweza kuhatarisha maisha yao na jamii inayowazungukana sanjari
na kuleta matatizo kwa taifa.
“Kila
inapotokea mtu yeyote akaona kitu ambacho hana uhakika nacho usikichukue kwa
masuala ya kupata dili utakuja kufa na kuua familia ni bora ukatoa
taarifa katika vyombo vya usalama”.Alisema Hongoa
Alitoa
mfano wa baadhi ya matukio kama hayo yaliyotokea hivi karibuni ambayo
yalisababisha madhara makubwa kwa watoto wilayani karagwe na Arusha na
kusababisha hasara kwa wazazi wao na hata taifa kwa kupoteza rasilimali
watu ambao wangekuwa wazalishaji wa uchumi wa taifa.
Awali
kabla kikosi hicho kutoka Tabora hakijawasili wilayani Ngara kulifika
kikosi cha wataalamu wa kambi ya JWTZ Biharamulo lakini uchunguzi wao
ulitia mashaka na kulazimika kutoa taarifa ngazi nyingine kwa ajili ya
uchunguzi wa kina licha ya baadhi ya wananchi na wanafunzi wa shule ya
sekondari ya kata ya kibimba kuonyesha utukutu wao kwa kukinyanyua kutoka
kilikotua na kukipeleka jirani zaidi na shule yao zaidi ya mita 500
Kitu
hicho kizito kilidondoka usiku wa manane na kuzama nusu yake ardhini kwa ukubwa
wa diameta 50 kilomita mbili nje ya uwanja wa ndege wa kijiji cha Ruganzo
ambapo baadhi ya raia walidhani kuwa ni Kimondo,kilichodondoka na
kusababisha mshindo mkubwa uliosikika wilaya nzima na nchi za jirani.
Akihutubia
wananchi Mwenyekiti wa kijiji cha Ruganzo kata ya kibimba wilaya ya
Ngara mkoani Kagera Salvatori Mbanyi alisema kuwa kitu hicho kilidondoka
kutoka angani na mshindo wake kuwashtua wananchi na asubuhi yake kilionwa na
watu karibu na mto Ruvubu unaopita kijiji humo kutoka mpakani mwa nchi ya
Burundi kuelekea Rusumo mpakani mwa Ngara na Rwanda.
Mbanyi
alisema kuwa mara baada ya wananchi kuona kilichosababisha mlipuko viongozi
walipeleka taarifa kwa jeshi la polisi pamoja na ofisi ya mkuu wa wilaya
kwa ajili ya kupata maelekezo na ufafanuzi zaidi ambapo kamati ya ulinzi
na usalama ya wilaya ilianza kazi yake .
Alisema kadri masaa yalivyosogea
asubuhi umbo lake liliongezeka na kutanuka kama vile kinataka kulipuka na
baadaye hali hiyo iliisha na baadhi ya wananchi walianza
kukisogelea na kukigusa kisha kujaribu kukihamisha huku
watoto na wanafunzi wakikinyofoa nyuzi zilizokifunika
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya
Ngara Costantine Kanyasu alisema kutokana na kitu hicho kuanguka eneo la wilaya
yake lilisababisha taharuki kubwa kwa wananchi ambapo baadhi yao waliamini kuwa
ni kombora la masafa marefu lililorushwa kutoka kutokana na vita vinavyoendelea
kwenye nchi ya DRC dhidi ya waasi wa 23 na majeshi la serikali.
Kamanda wa polisi mkoani kagera
Philip Karangi aliwataka wananchi wa ngara kushilikiana na vyombo vya ulinzi na
usalama mkoani humo kwa kutoa taarifa za kiusalama mapema ili kuondoa madhara
yanayoweza kujitokeza badala ya baadhi ya wananchi kufanya kazi za kitaalamu
zisizowahusu hali inayoweza kusababisha madhara makubwa kutokana na uzembe.
Kikosi cha Brigedia ya Faru Makao
makuu ya Tabora kinasimamia mikoa minane ya Kanda ya ziwa ikiwa ni
Tabora,Shinyanga,Simiyu,Mara,Mwanza,Geita,Kagera na Kigoma.
Mwisho.
M4C YAITESA CCM KARAGWE
Na: Magreth Chaba
Mikutano ya vuguvugu la mabadiliko (M4C) inayofanywa na
chama cha Demokrasia na maendeleo (Chadema) Wilayani Karagwe ikiongozwa na
katibu Mkuu wa chama hicho Daktari Wilbroad Slaa imezoa makada zaidi ya 300
wa CCM na CUF.
Makada hao ni mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Wilaya, na mjumbe wa
mkutano Mkuu wa (CCM) kata ya kanoni Prince Bashaija Rwazo ambaye
pia ni mtoto wa katibu mwenezi wa (CCM) Mstaafu Mkoa wa Kagera na diwani
wa kata ya Kanoni (CCM) Sabby Rwazo, na Mwenyekiti wa chama cha (CUF)
kata ya Nyakahanga Enock Gabagambi ambao wamekabidhi kadi za vyama vyao vya
zamani na kukabidhiwa kadi za (Chadema) na katibu wa chama hicho.
Ukiacha wanachama hao, zaidi ya wanachama 600 wamehama vyama vyao
na kuhamia chadema, ambapo ilielezwa kuwa wanachama saba kutoka kata ya
Nyakahanga kupitia Chama cha (CUF) wamekabidhi kadi za chama
hicho na kuhamia chama cha demokrasia na maendeleo (Chadema), kuwa pia
wanachama 324 kutoka cham acha mapinduzi (CCM) wamekabidhi kadi
zao.
Kwa mjibu wa katibu wa Chadema wilaya ya karagwe Geofrey Nguma
alisema kuwa wanachama hao walitoka katika kata ya Nyakahanga, Kibondo,
Nyakabanga na kata nyingine kuwa ni Bweranyange, Kiruruma, Nyabiyonza, RUGERA,
Ihanda na Kayanga.
Aliongeza kuwa pamoja na baadhi ya makada hao waliokabidhi kadi
zao kuwa zaidi ya wanachama wapya 600 wamejiunga na chama chake na kukata kadi
ambapo katibu Mkuu wa chama hicho alishiriki kukabidhi kadi kwa wanachama hao.
Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara jana mjini Kayanga
uliofanyika katika uwanja wa michezo mjini humo, muda mfupi baada ya katibu
mkuu wa chedema kumkabidhi kadi Rwazo alisema ameamua kujiunga na chama hicho
baada ya kuona chama cha mapinduzi hakina mwelekeo wa kuwasaidia watanzania
tofauti na kuwanyanyasa na kukithiri kwa vitendo vya rushwa.
“Nimeona nihamie huku maana pamoja na kuwa kada mzuri wa CCM
sioni mabadiliko yoyote zaidi ya majungu, rushwa na manyanyaso tunayotendewa na
wenye chama nikiwa na maana ccm niyawachache wenye pesa ukitaka kuria akili kaa
CCM” Alisema Rwazo.
Kwa upande wake Kiongozi wa (M4C) kutika makao makuu ambaye
pia ni katibu wa chadema Dodoma mjini Steven Massawe aliwataka wananchi kuachana na CCM,
kwani kwa miaka yote imeshindwa kuwaletea maendeleo na baadala yake wachukue hatua
ili kuiondoa madarakani, vinginevyo vizazi vijavyo vitakuta mashimo.
Tuesday, October 23, 2012
WAKRISTO GEITA WACHARUKA WADAI HAWAKO TAYARI KUCHOMEWA
MAKANISA
Na
MAGRETH CHABA
|
UMOJA wa makanisa ya kikristo ya Katoro wilayani Geita na
Buseresere wilayani Chato,mkoani Geita umecharuka na kulaani kitendo cha hivi
karibuni kilichofanywa na baadhi ya waumini wa dini ya kiislamu cha kuchoma
moto makanisa na kuharibu mali za wakiristo.
Kitendo hicho kilisababisha vurugu kubwa zilizotokea oktoba 12 mwaka huu Mbagala Kizuiani jijini Dar es Salaam ambapo makanisa saba yalichomwa moto kutokana na kitendo kinachodaiwa na mtoto mwenye umri wa miaka 14 kukojolea Quran. Umoja huo umetoa tamko kuhusiana na kitendo hicho katika mkutano wa uliofanyika juzi mjini Katoro na kuwakutanisha waumini wa madhehebu mbalimbali ya kikristo pamoja na viongozi wao. Akitoa tamko hilo mwenyekiti wa umoja huo,Mchungaji Joseph Mwanzalima Hewa,alisema serikali ikishindwa kudhibiti matukio ya vurugu za waislamu kujichukulia sheria mkononi kutokana na udini taifa halitakuwa na amani. Alisema kuna hatari ya taifa,linaweza kuingia katika umwagaji wa damu kwani kitendo hicho hakivumiliki kwa wakristo kuzidi kupumbazika kwa kuharibiwa mali zao. Hewa alisema zaidi ya biblia 50 ziliwahi kuchomwa moto lakini wakristo hawakuchukua hatua zozote dhidi ya wahusika wala hakuna msikiti uliochomwa moto na kwamba hakuna vurugu zilizotokea na hivyo kuhoji uhalali wa waislamu kuiweka nchi kwenye rehani ya vita ya kidini. Alisema serikali inapaswa kuingilia kati kukomesha matukio hayo yanayofanywa na baadhi ya makundi ya waumini wa dini ya kiislamu ili nchi iendelee kuwa kisiwa cha amani. Aidha alisema kama serikali itashindwa kudhibiti matukio hayo,hawatavumilia kuendelea kuharibiwa makanisa yao na kudai kuwa wako tayari kufa wakitetea haki zao. Kiongozi huyo aliongeza kuwa waliohusika katika matukio hayo wanapaswa kuchukulia hatua kali za kisheria akiwemo kinara wa kikundi cha Uamsho kisiwani Zanzibar Sheikh Farid Hadi Ahmed. ''Serikali imekuwa ikiwakumbatia waislamu sasa tunasema yatosha,hatuwezi kuona mali zetu zinaharibiwa,kama itakuwa kimiya katika hili nchi itaingia katika vurugu kubwa na vita kutokana na udini ulioanza kujipenyeza''alisema Hewa. Naye aliyewahi kuwa mwenyekiti wa umoja huo Isaya Ikili alisema anasikitishwa na watendaji wa kata pamoja na viongozi wa serikali kushindwa kuhudhuria katika mkutano huo licha kupewa mwaliko ili kujua matamko yao. Alisema wako tayari kupambana na maadui wao wanaoharibu makanisa yao na kwamba polisi wasiingilie vurugu hizo kama serikali itashindwa kuyadhibiti. MWISHO. |
MW/KITI CCM GEITA APIGWA STOP MGODINI AKIENDA KUZINDUA
KAMPENI
|
WAKRISTO GEITA WACHARUKA WADAI HAWAKO TAYARI KUCHOMEWA MAKANISA
WAKRISTO GEITA WACHARUKA WADAI HAWAKO TAYARI KUCHOMEWA
MAKANISA
Na
MAGRETH CHABA
|
UMOJA wa makanisa ya kikristo ya Katoro wilayani Geita na
Buseresere wilayani Chato,mkoani Geita umecharuka na kulaani kitendo cha hivi
karibuni kilichofanywa na baadhi ya waumini wa dini ya kiislamu cha kuchoma
moto makanisa na kuharibu mali za wakiristo.
Kitendo hicho kilisababisha vurugu kubwa zilizotokea oktoba 12 mwaka huu Mbagala Kizuiani jijini Dar es Salaam ambapo makanisa saba yalichomwa moto kutokana na kitendo kinachodaiwa na mtoto mwenye umri wa miaka 14 kukojolea Quran. Umoja huo umetoa tamko kuhusiana na kitendo hicho katika mkutano wa uliofanyika juzi mjini Katoro na kuwakutanisha waumini wa madhehebu mbalimbali ya kikristo pamoja na viongozi wao. Akitoa tamko hilo mwenyekiti wa umoja huo,Mchungaji Joseph Mwanzalima Hewa,alisema serikali ikishindwa kudhibiti matukio ya vurugu za waislamu kujichukulia sheria mkononi kutokana na udini taifa halitakuwa na amani. Alisema kuna hatari ya taifa,linaweza kuingia katika umwagaji wa damu kwani kitendo hicho hakivumiliki kwa wakristo kuzidi kupumbazika kwa kuharibiwa mali zao. Hewa alisema zaidi ya biblia 50 ziliwahi kuchomwa moto lakini wakristo hawakuchukua hatua zozote dhidi ya wahusika wala hakuna msikiti uliochomwa moto na kwamba hakuna vurugu zilizotokea na hivyo kuhoji uhalali wa waislamu kuiweka nchi kwenye rehani ya vita ya kidini. Alisema serikali inapaswa kuingilia kati kukomesha matukio hayo yanayofanywa na baadhi ya makundi ya waumini wa dini ya kiislamu ili nchi iendelee kuwa kisiwa cha amani. Aidha alisema kama serikali itashindwa kudhibiti matukio hayo,hawatavumilia kuendelea kuharibiwa makanisa yao na kudai kuwa wako tayari kufa wakitetea haki zao. Kiongozi huyo aliongeza kuwa waliohusika katika matukio hayo wanapaswa kuchukulia hatua kali za kisheria akiwemo kinara wa kikundi cha Uamsho kisiwani Zanzibar Sheikh Farid Hadi Ahmed. ''Serikali imekuwa ikiwakumbatia waislamu sasa tunasema yatosha,hatuwezi kuona mali zetu zinaharibiwa,kama itakuwa kimiya katika hili nchi itaingia katika vurugu kubwa na vita kutokana na udini ulioanza kujipenyeza''alisema Hewa. Naye aliyewahi kuwa mwenyekiti wa umoja huo Isaya Ikili alisema anasikitishwa na watendaji wa kata pamoja na viongozi wa serikali kushindwa kuhudhuria katika mkutano huo licha kupewa mwaliko ili kujua matamko yao. Alisema wako tayari kupambana na maadui wao wanaoharibu makanisa yao na kwamba polisi wasiingilie vurugu hizo kama serikali itashindwa kuyadhibiti. MWISHO. |
MW/KITI CCM GEITA APIGWA STOP MGODINI AKIENDA KUZINDUA
KAMPENI
|
Subscribe to:
Posts (Atom)
