Saturday, December 15, 2012

KITUO CHA POLISI MUGOMA NGARA CHATEKEKETEA,NA WATU WATATU WADAIWA KUPOTEZA MAISHA







Kituo cha police Mugoma wilayani ngara mkoani kagera kikiwa kimechomwa moto na wananchi,baada ya asikari police kumuua mkazi mmoja kwa risasi na hivyo kusababisha vurugu zilizopelekea asikari wawili Cpl Paschal & Pc Alex.

Mungu azipumzishe kwa amani roho zao marehemu waliotokana na tukio hili

Monday, November 26, 2012

JWTZ LA TOA UFAFANUZI MLIPUKO NGARA




JWTZ LATOA UFAFANUZI MLIPUKO NGARA.

Na Magreth chaba ,Ngara
JESHI la wananchi wa Tanzania  JWTZ  kikosi cha Faru makao makuu ya  Tabora limetoa ufafanuzi juu ya msihndo mkubwa uliojitokeza wilayani ngara mkoani kagera na kusababisha baadhi ya wananchi kuyakimbia kwa muda makazi yao kwa kuhofia maisha kutokana na kile walichodai bomu lilidondoka kwenye kijiji cha Ruganzo wilayani humo.

Katika tukio hilo ambalo lilitokea usiku wa Novemba 22 majira ya saa nane lilisababisha baadhi ya wakazi wa wilaya ya ngara kuishi kwa hofu kubwa kutokana kitu kisichofahamika kudondoka toka angani na kusababisha mshindo mkubwa mithili ya tetemeko la ardhi hali iliyopelekea baadhi ya nyumba kupata nyufa.

Kufuatia hali hiyo kiongozi wa kikosi cha JWTZ  Mnadhimu mkuu wa mafunzo  na utendaji wa kivita Brigedia ya Faru Kanali Simon Lali Hongoa amelazimika kutoa ufafanuzi wa kitu hicho baada ya wataalamu wa mabomu kufika kijiji cha Ruganzo kata ya Kibimba wilayani Ngara na kufanya uchunguzi wa kina baada ya kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya hiyo kushindwa kubaini ni kitu gani pamoja na madhara yake.
Kanali Hongoa alikanusha vikali madai ya wananchi wa ngara kuwa kitu kilichodondoka wilayani humo kilikuwa ni bomu la kivita na kudai kuwa maneno hayo hayakuwa na ukweli wowote kwa kuwa kilichodondoka kilikuwa ni kipande cha setelaiti iliyokuwa ikisafiri angani na inahofiwa kiliishiwa nguvu na kudodoka  katika eneo hilo.

Aidha alidai kuwa uchunguzi wa kitaalamu umebainisha kuwa setelaiti hiyo haina madhara yoyote na wala haikutoka uelekeo wa nchi jirani zinazoendelea na migogoro ya kivita kama baadhi ya maelezo ya wananchi wa wilaya hiyo walivyodai.
Hangoa alisema pamoja na kutokuwepo madhara kila mwananchi anatakiwa kuchukua tahadhari ya kubeba vitu wasivyokuwa na uhakika navyo wakilenga kutaka kupata utajiri wa haraka ambao unaweza kuhatarisha maisha yao na jamii inayowazungukana sanjari na kuleta matatizo kwa taifa.
“Kila inapotokea mtu yeyote akaona kitu ambacho hana uhakika nacho usikichukue kwa masuala ya kupata dili utakuja kufa na kuua familia  ni bora ukatoa taarifa katika vyombo vya usalama”.Alisema Hongoa
 Alitoa mfano wa baadhi ya matukio kama hayo yaliyotokea hivi karibuni ambayo yalisababisha madhara makubwa kwa watoto  wilayani karagwe na Arusha na kusababisha  hasara kwa wazazi wao na hata taifa kwa kupoteza rasilimali watu ambao wangekuwa wazalishaji wa uchumi wa taifa.
Awali kabla  kikosi hicho kutoka Tabora hakijawasili wilayani Ngara kulifika kikosi  cha wataalamu wa kambi ya JWTZ Biharamulo lakini uchunguzi wao ulitia mashaka na kulazimika kutoa taarifa ngazi nyingine kwa ajili ya uchunguzi wa kina licha ya baadhi ya wananchi na wanafunzi wa shule ya sekondari ya kata ya kibimba kuonyesha utukutu wao kwa kukinyanyua kutoka kilikotua na kukipeleka jirani zaidi na  shule yao zaidi ya mita 500
Kitu hicho kizito kilidondoka usiku wa manane na kuzama nusu yake ardhini kwa ukubwa wa diameta 50 kilomita mbili nje ya uwanja wa ndege wa kijiji cha  Ruganzo ambapo baadhi ya raia  walidhani kuwa ni Kimondo,kilichodondoka na kusababisha mshindo mkubwa uliosikika wilaya nzima na  nchi za jirani.
Akihutubia wananchi Mwenyekiti wa kijiji cha Ruganzo  kata ya kibimba wilaya ya  Ngara mkoani Kagera Salvatori Mbanyi  alisema kuwa kitu hicho kilidondoka kutoka angani na mshindo wake kuwashtua wananchi na asubuhi yake kilionwa na watu karibu na mto Ruvubu unaopita kijiji humo kutoka mpakani mwa nchi ya Burundi kuelekea Rusumo mpakani mwa Ngara na Rwanda.
Mbanyi alisema kuwa mara baada ya wananchi kuona kilichosababisha mlipuko viongozi walipeleka taarifa kwa  jeshi la polisi pamoja na ofisi ya mkuu wa wilaya kwa ajili ya kupata maelekezo na ufafanuzi zaidi  ambapo kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ilianza kazi yake .
Alisema kadri masaa yalivyosogea asubuhi umbo lake liliongezeka na kutanuka kama vile kinataka kulipuka na baadaye hali hiyo iliisha na  baadhi ya wananchi  walianza kukisogelea na kukigusa  kisha  kujaribu kukihamisha huku  watoto na wanafunzi wakikinyofoa nyuzi zilizokifunika                  

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Ngara Costantine Kanyasu alisema kutokana na kitu hicho kuanguka eneo la wilaya yake lilisababisha taharuki kubwa kwa wananchi ambapo baadhi yao waliamini kuwa ni kombora la masafa marefu lililorushwa kutoka kutokana na vita vinavyoendelea kwenye nchi ya DRC dhidi ya waasi wa 23 na majeshi la serikali.

Kamanda wa polisi mkoani kagera Philip Karangi aliwataka wananchi wa ngara kushilikiana na vyombo vya ulinzi na usalama mkoani humo kwa kutoa taarifa za kiusalama mapema ili kuondoa madhara yanayoweza kujitokeza badala ya baadhi ya wananchi kufanya kazi za kitaalamu zisizowahusu hali inayoweza kusababisha madhara makubwa kutokana na uzembe.

Kikosi cha Brigedia ya Faru Makao makuu ya Tabora kinasimamia mikoa minane ya Kanda ya ziwa ikiwa ni Tabora,Shinyanga,Simiyu,Mara,Mwanza,Geita,Kagera na Kigoma.
                                                                          Mwisho.

M4C YAITESA CCM KARAGWE




Na: Magreth Chaba

Mikutano ya vuguvugu la mabadiliko (M4C) inayofanywa na chama cha Demokrasia na maendeleo (Chadema) Wilayani Karagwe ikiongozwa na katibu Mkuu wa chama hicho Daktari Wilbroad Slaa imezoa makada zaidi ya 300 wa CCM na CUF.
Makada hao ni mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Wilaya, na mjumbe wa mkutano Mkuu wa (CCM) kata ya kanoni Prince Bashaija  Rwazo ambaye pia ni mtoto wa katibu mwenezi wa (CCM) Mstaafu Mkoa wa Kagera na diwani wa kata ya Kanoni (CCM) Sabby Rwazo, na Mwenyekiti wa chama cha (CUF) kata ya Nyakahanga Enock Gabagambi ambao wamekabidhi kadi za vyama vyao vya zamani na kukabidhiwa kadi za (Chadema) na katibu wa chama hicho.

Ukiacha wanachama hao, zaidi ya wanachama 600 wamehama vyama vyao na kuhamia chadema, ambapo ilielezwa kuwa wanachama saba kutoka kata ya Nyakahanga  kupitia  Chama cha (CUF) wamekabidhi kadi za chama hicho na kuhamia chama cha demokrasia  na maendeleo (Chadema), kuwa pia wanachama 324 kutoka cham acha mapinduzi (CCM) wamekabidhi kadi zao.
Kwa mjibu wa katibu wa Chadema wilaya ya karagwe Geofrey Nguma alisema kuwa wanachama hao walitoka katika kata ya Nyakahanga, Kibondo, Nyakabanga na kata nyingine kuwa ni Bweranyange, Kiruruma, Nyabiyonza, RUGERA, Ihanda na Kayanga.
Aliongeza kuwa pamoja na baadhi ya makada hao waliokabidhi kadi zao kuwa zaidi ya wanachama wapya 600 wamejiunga na chama chake na kukata kadi ambapo katibu Mkuu wa chama hicho alishiriki kukabidhi kadi kwa wanachama hao.

Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara jana mjini Kayanga uliofanyika katika uwanja wa michezo mjini humo, muda mfupi baada ya katibu mkuu wa chedema kumkabidhi kadi Rwazo alisema ameamua kujiunga na chama hicho baada ya kuona chama cha mapinduzi hakina mwelekeo wa kuwasaidia watanzania tofauti na kuwanyanyasa na kukithiri kwa vitendo vya rushwa.
“Nimeona nihamie huku maana pamoja na kuwa kada mzuri wa CCM sioni mabadiliko yoyote zaidi ya majungu, rushwa na manyanyaso tunayotendewa na wenye chama nikiwa na maana ccm niyawachache wenye pesa ukitaka kuria akili kaa CCM” Alisema  Rwazo.

Kwa upande wake Kiongozi wa (M4C) kutika makao makuu ambaye pia ni katibu wa chadema Dodoma mjini Steven Massawe  aliwataka wananchi kuachana na CCM, kwani kwa miaka yote imeshindwa kuwaletea maendeleo na baadala yake wachukue hatua ili kuiondoa madarakani, vinginevyo vizazi vijavyo vitakuta mashimo. 

Tuesday, October 23, 2012



WAKRISTO GEITA WACHARUKA WADAI HAWAKO TAYARI KUCHOMEWA MAKANISA
Na
MAGRETH CHABA
UMOJA wa makanisa ya kikristo ya Katoro wilayani Geita na Buseresere wilayani Chato,mkoani Geita umecharuka na kulaani kitendo cha hivi karibuni kilichofanywa na baadhi ya waumini wa dini ya kiislamu cha kuchoma moto makanisa na kuharibu mali za wakiristo.

Kitendo hicho kilisababisha vurugu kubwa zilizotokea  oktoba 12 mwaka huu Mbagala Kizuiani jijini Dar es Salaam ambapo makanisa saba yalichomwa moto kutokana na kitendo kinachodaiwa na mtoto mwenye umri wa miaka 14 kukojolea Quran.

Umoja huo umetoa tamko kuhusiana na kitendo hicho katika mkutano wa uliofanyika juzi mjini Katoro na kuwakutanisha waumini wa madhehebu mbalimbali ya kikristo pamoja na viongozi wao.

Akitoa tamko hilo mwenyekiti wa umoja huo,Mchungaji Joseph Mwanzalima Hewa,alisema serikali ikishindwa kudhibiti matukio ya vurugu za waislamu kujichukulia sheria mkononi kutokana na udini taifa halitakuwa na amani.

Alisema kuna hatari ya taifa,linaweza kuingia katika umwagaji wa damu kwani kitendo hicho hakivumiliki kwa wakristo kuzidi kupumbazika kwa kuharibiwa mali zao.

Hewa alisema zaidi ya biblia 50 ziliwahi kuchomwa moto lakini wakristo hawakuchukua hatua zozote dhidi ya wahusika wala hakuna msikiti uliochomwa moto na kwamba hakuna vurugu zilizotokea na hivyo kuhoji uhalali wa waislamu kuiweka nchi kwenye rehani ya vita ya kidini.

Alisema serikali inapaswa kuingilia kati kukomesha matukio hayo yanayofanywa na baadhi ya makundi ya waumini wa dini ya kiislamu ili nchi iendelee kuwa kisiwa cha amani.

Aidha alisema kama serikali itashindwa kudhibiti matukio hayo,hawatavumilia kuendelea kuharibiwa makanisa yao na kudai kuwa wako tayari kufa wakitetea haki zao.

Kiongozi huyo aliongeza kuwa waliohusika katika matukio hayo wanapaswa kuchukulia hatua kali za kisheria akiwemo kinara wa kikundi cha Uamsho kisiwani Zanzibar Sheikh Farid Hadi Ahmed.

''Serikali imekuwa ikiwakumbatia waislamu sasa tunasema yatosha,hatuwezi kuona mali zetu zinaharibiwa,kama itakuwa kimiya katika hili nchi itaingia katika vurugu kubwa na vita kutokana na udini ulioanza kujipenyeza''alisema Hewa.

Naye aliyewahi kuwa mwenyekiti wa umoja huo Isaya Ikili alisema anasikitishwa na watendaji wa kata pamoja na viongozi wa serikali kushindwa kuhudhuria katika mkutano huo licha kupewa mwaliko ili kujua matamko yao.

Alisema wako tayari kupambana na maadui wao wanaoharibu makanisa yao na kwamba polisi wasiingilie vurugu hizo kama serikali itashindwa kuyadhibiti.
                                                                            MWISHO.

MW/KITI CCM GEITA APIGWA STOP MGODINI AKIENDA KUZINDUA KAMPENI
Na                           
Magreth chaba

VIGOGO wa chama cha mapinduzi(ccm)mkoani Geita waliochaguliwa hivi karibuni ,akiwemo mwenyekiti wa mkoani ,Joseph Msukuma wameonja machungu ya mgodi wa dhahabu wa Geita (GGM)baada ya msafara wao kuzuiliwa kwa muda wakati wakielekea kwenye uzinduzi wa kampeni za uchaguzi mdogo.

Tukio la kuzuiliwa kwa viongozi hao lilitokea jana mchana saa 7:03 kutokana na kile kilichodaiwa na walinzi wa mgodi huo kampuni ya G4S waliokuwa wamefura hawakuwa na taarifa za viongozi hao kupita mgodini hapo kitendo kilichosababisha majibizano makali ya maneno kati ya walinzi hao na vigogo hao.

Mwenyekiti huyo alikumbwa na kizazaa hicho akiwa na katibu wa itikadi na uenezi mkoa Said Kalidushi na katibu wa uchumi na fedha mkoa Malugu Mwendesha walipokuwa wakielekea katika kuzindua  kampeni za uchaguzi mdogo wa kata ya Lwezera tarafa ya Bugando.

Baada ya kuzuiliwa Msukuma alijitambulisha kwa walinzi kuwa ni mwenyekiti wa ccm mkoa huku akiwaonyesha bendera ya chama iliyokuwa ikipepea kwenye gari lake lenye namba za usajili T 164 AFQ aina ya Toyota V-8 lakini walinzi walisema wao wanafuata sheria za uongozi wa mgodi huo na kwamba hawakuwa tayari kuruhu kupita kwa kuwa hawakupewa na taarifa.

Msukuma alisikika akiwakaripia maneno walinzi hao’’serikali Unayoitaka wewe ni ipi,tueleweshe ama unataka ya chama gani huoni hata bendera,kila siku napita hapa huwa hamnioni na hili gari ’’

Naye mlinzi mmoja alisikika akisema’’sisi tunafuata taratibu zilizopo,kwani mnaelekea wapi?,sisi hata kama ni kiongozi wa serikali anapofika hapa huwa tunataarifiwa lakini sasa hatuJajulishwa’’

Kufuatia maneno hayo ya mwenyekiti,mlinzi mmoja alijitokeza na kulazimika kupiga simu mgodini kuuliza kuhusu kumruhusu kupita ambapo wakati akifanya mawasiliano hayo mlinzi huyo alisikika akizitaya namba za gari hilo.

Mlinzi huyo baada ya kuwasiliana na uongozi wa mgodi huo na kuruhusiwa viongozi hao kupita saa 7:25,mmoja wao alisema’’tunaomba samahani kama tumewachelewesha sisi tunafuata taratibu za uongozi wa mgodi’’.

Aidha akiwa katika uzinduzi wa kampeni hizo mwenyekiti wa aliwataka wananchi wa kata hiyo kumchagua mgombea wa ccm Misango Jeremiah ili kuwaletea maendeleo katika kata hiyo ikiwemo huduma ya afya barabara na ofisi ya kata hiyo.

Kampeni za uchaguzi huo unaotarajia kufanyika oktoba 28 mwaka huu unakuja kufuatia kifo cha aliyekuwa diwani wa kata hiyo Anatori Mkufu aliyefariki februari 23,mwaka huu kwa ajali ya gari akiwa jijini Mwanza.
                                                                    MWISHO.

WAKRISTO GEITA WACHARUKA WADAI HAWAKO TAYARI KUCHOMEWA MAKANISA



WAKRISTO GEITA WACHARUKA WADAI HAWAKO TAYARI KUCHOMEWA MAKANISA
Na
MAGRETH CHABA
UMOJA wa makanisa ya kikristo ya Katoro wilayani Geita na Buseresere wilayani Chato,mkoani Geita umecharuka na kulaani kitendo cha hivi karibuni kilichofanywa na baadhi ya waumini wa dini ya kiislamu cha kuchoma moto makanisa na kuharibu mali za wakiristo.

Kitendo hicho kilisababisha vurugu kubwa zilizotokea  oktoba 12 mwaka huu Mbagala Kizuiani jijini Dar es Salaam ambapo makanisa saba yalichomwa moto kutokana na kitendo kinachodaiwa na mtoto mwenye umri wa miaka 14 kukojolea Quran.

Umoja huo umetoa tamko kuhusiana na kitendo hicho katika mkutano wa uliofanyika juzi mjini Katoro na kuwakutanisha waumini wa madhehebu mbalimbali ya kikristo pamoja na viongozi wao.

Akitoa tamko hilo mwenyekiti wa umoja huo,Mchungaji Joseph Mwanzalima Hewa,alisema serikali ikishindwa kudhibiti matukio ya vurugu za waislamu kujichukulia sheria mkononi kutokana na udini taifa halitakuwa na amani.

Alisema kuna hatari ya taifa,linaweza kuingia katika umwagaji wa damu kwani kitendo hicho hakivumiliki kwa wakristo kuzidi kupumbazika kwa kuharibiwa mali zao.

Hewa alisema zaidi ya biblia 50 ziliwahi kuchomwa moto lakini wakristo hawakuchukua hatua zozote dhidi ya wahusika wala hakuna msikiti uliochomwa moto na kwamba hakuna vurugu zilizotokea na hivyo kuhoji uhalali wa waislamu kuiweka nchi kwenye rehani ya vita ya kidini.

Alisema serikali inapaswa kuingilia kati kukomesha matukio hayo yanayofanywa na baadhi ya makundi ya waumini wa dini ya kiislamu ili nchi iendelee kuwa kisiwa cha amani.

Aidha alisema kama serikali itashindwa kudhibiti matukio hayo,hawatavumilia kuendelea kuharibiwa makanisa yao na kudai kuwa wako tayari kufa wakitetea haki zao.

Kiongozi huyo aliongeza kuwa waliohusika katika matukio hayo wanapaswa kuchukulia hatua kali za kisheria akiwemo kinara wa kikundi cha Uamsho kisiwani Zanzibar Sheikh Farid Hadi Ahmed.

''Serikali imekuwa ikiwakumbatia waislamu sasa tunasema yatosha,hatuwezi kuona mali zetu zinaharibiwa,kama itakuwa kimiya katika hili nchi itaingia katika vurugu kubwa na vita kutokana na udini ulioanza kujipenyeza''alisema Hewa.

Naye aliyewahi kuwa mwenyekiti wa umoja huo Isaya Ikili alisema anasikitishwa na watendaji wa kata pamoja na viongozi wa serikali kushindwa kuhudhuria katika mkutano huo licha kupewa mwaliko ili kujua matamko yao.

Alisema wako tayari kupambana na maadui wao wanaoharibu makanisa yao na kwamba polisi wasiingilie vurugu hizo kama serikali itashindwa kuyadhibiti.
                                                                            MWISHO.

MW/KITI CCM GEITA APIGWA STOP MGODINI AKIENDA KUZINDUA KAMPENI
Na                           
Magreth chaba

VIGOGO wa chama cha mapinduzi(ccm)mkoani Geita waliochaguliwa hivi karibuni ,akiwemo mwenyekiti wa mkoani ,Joseph Msukuma wameonja machungu ya mgodi wa dhahabu wa Geita (GGM)baada ya msafara wao kuzuiliwa kwa muda wakati wakielekea kwenye uzinduzi wa kampeni za uchaguzi mdogo.

Tukio la kuzuiliwa kwa viongozi hao lilitokea jana mchana saa 7:03 kutokana na kile kilichodaiwa na walinzi wa mgodi huo kampuni ya G4S waliokuwa wamefura hawakuwa na taarifa za viongozi hao kupita mgodini hapo kitendo kilichosababisha majibizano makali ya maneno kati ya walinzi hao na vigogo hao.

Mwenyekiti huyo alikumbwa na kizazaa hicho akiwa na katibu wa itikadi na uenezi mkoa Said Kalidushi na katibu wa uchumi na fedha mkoa Malugu Mwendesha walipokuwa wakielekea katika kuzindua  kampeni za uchaguzi mdogo wa kata ya Lwezera tarafa ya Bugando.

Baada ya kuzuiliwa Msukuma alijitambulisha kwa walinzi kuwa ni mwenyekiti wa ccm mkoa huku akiwaonyesha bendera ya chama iliyokuwa ikipepea kwenye gari lake lenye namba za usajili T 164 AFQ aina ya Toyota V-8 lakini walinzi walisema wao wanafuata sheria za uongozi wa mgodi huo na kwamba hawakuwa tayari kuruhu kupita kwa kuwa hawakupewa na taarifa.

Msukuma alisikika akiwakaripia maneno walinzi hao’’serikali Unayoitaka wewe ni ipi,tueleweshe ama unataka ya chama gani huoni hata bendera,kila siku napita hapa huwa hamnioni na hili gari ’’

Naye mlinzi mmoja alisikika akisema’’sisi tunafuata taratibu zilizopo,kwani mnaelekea wapi?,sisi hata kama ni kiongozi wa serikali anapofika hapa huwa tunataarifiwa lakini sasa hatuJajulishwa’’

Kufuatia maneno hayo ya mwenyekiti,mlinzi mmoja alijitokeza na kulazimika kupiga simu mgodini kuuliza kuhusu kumruhusu kupita ambapo wakati akifanya mawasiliano hayo mlinzi huyo alisikika akizitaya namba za gari hilo.

Mlinzi huyo baada ya kuwasiliana na uongozi wa mgodi huo na kuruhusiwa viongozi hao kupita saa 7:25,mmoja wao alisema’’tunaomba samahani kama tumewachelewesha sisi tunafuata taratibu za uongozi wa mgodi’’.

Aidha akiwa katika uzinduzi wa kampeni hizo mwenyekiti wa aliwataka wananchi wa kata hiyo kumchagua mgombea wa ccm Misango Jeremiah ili kuwaletea maendeleo katika kata hiyo ikiwemo huduma ya afya barabara na ofisi ya kata hiyo.

Kampeni za uchaguzi huo unaotarajia kufanyika oktoba 28 mwaka huu unakuja kufuatia kifo cha aliyekuwa diwani wa kata hiyo Anatori Mkufu aliyefariki februari 23,mwaka huu kwa ajali ya gari akiwa jijini Mwanza.
                                                                    MWISHO.