Thursday, June 14, 2012

MADIWANI BIHARAMULO WALITUHUMU JESHI LA POLIS


Na
Magreth Chaba
 Biharamulo

MADIWANI wa halmashauri ya wilaya ya Biharamulo mkoani Kagera wamelituhumu jeshi la polisi wilayani humo kujihusisha na uharibifu wa mazingira baada ya kufumbia macho vitendo vya uvushwaji wa mkaa na magogo ya miti(Mbilimbi) kinyume cha sheria,ambapo mazao hayo husafirishwa na watu wanaosadikiwa wahamiaji haramu wa nje ya nchi na kuyapeleka nchini Rwanda.
 
Askari waliotuhumiwa ni wa kituo kidogo cha Nyakanazi wilayani humo ambapo wanadaiwa kushirikiana na wavunaji haramu wa raslimali ya misitu kutoka nchini Rwanda ambao huvusha mazao hayo kwa njia ya malori kupitia kizuizi kilichopo kwenye kituo hicho cha polisi licha ya kujua wazi kuwa kufanya hivyo ni kuhujumu uchumi wa taifa.
 
Hatua hiyo imekuja baada ya diwani wa kata ya Kalenge Gabriel Kakulu kutaka kujua chanzo cha uharibifu mkubwa wa misitu katika msitu wa hifadhi ya taifa wa Biharamulo upande wa kata ya Nyantakara ambapo eneo kubwa limeharibiwa vibaya baada ya wavamizi wa ndani na nje ya nchi kuingia ndani yake kinyume cha sheria na kujihusisha na ukataji miti ya kupasua mbao,uchomaji mkaa,kilimo na uchimbaji madini.
 
Kutokana na hali hiyo Kakulu alidai kutokuwa na imani na baadhi ya watendaji wa idara ya misitu waliopo kwenye kata hiyo pamoja na jeshi la polisi wilayani humo  kushindwa kudhibiti uvushwaji wa mazao hayo kinyume cha sheria licha ya mazao hayo kusafirishwa kupitia kizuizi cha polisi kilichopo jirani kabisa na kituo kidogo cha Nyakanazi ambapo yamekuwa yakipelekwa nchini Rwanda pasipo kutozwa ushuru hali inayopelekea halmashauri hiyo kupoteza mapato mengi kila kukicha.
 
Alisema halmashauri ya Biharamulo ilitarajia kukusanya shilingi Milioni tatu katika robo ya mwaka katika bejeti yake 2011/12 katika mapato yake ya ndani lakini kutokana na baadhi ya

No comments:

Post a Comment